Thursday, January 31, 2013

BWALYA ASIKITISHWA NA KUTOLEWA KWA ZAMBIA.

RAIS wa Shirikisho la Soka la Zambia, Kalusha Bwalya amesema amesikitishwa na matokeo ya timu ya taifa ya nchi hiyo yaliyopelekea kuvuliwa ubingwa wao katika hatua ya makundi ya michuano ya Mataifa ya Afrika inayoendelea. Zambia walilazimishwa sare ya bila ya kufungana na Burkina Faso katika mchezo wao wa mwisho wa kundi C uliochezwa katika Uwanja wa Mbombela na matokeo hayo yalishindwa kuwavusha kwenda robo fainali baada ya Nigeria kuifunga Ethiopia kwa mabao 2-0 kwenye mchezo mwingine wa kundi hilo uliochezwa katika Uwanja wa Royal Bafokeng, Rustenburg. Kalusha aliuambia mtandao wa shirikisho hilo kuwa wachezaji wa timu hiyo inabidi wajilaumu wenyewe kwa kutolewa mapema kwasababu hakuna timu yoyote kwenye mashindano hayo iliyopata maandalizi mazuri kama wao. Kalusha ambaye aliwahi kuwa mchezaji nyota wan chi hiyo amesema waliiandaa timu kwa muda wa kutosha na mategemeo yao ilikuwa ni kufika mbali zaidi ikiwezekana kutetea taji hilo lakini imeshindikana. Kwasasa Kalusha amesema inabidi wasahau michuano hiyo na kuhakikisha wanajiandaa vyema zaidi ili waweze kukata tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Brazil 2014.

No comments:

Post a Comment