Thursday, January 31, 2013

NFF YAWAJAZA MAPESA WACHEZAJI SUPER EAGLES.

WACHEZAJI wa timu ya taifa ya Nigeria, Super Eagles wamepokea posho ya dola 30,000 kila mmoja kutoka kwa Shirikisho la Soka nchini humo-NFF baada ya kufanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon. Nigeria iliigaragaza Ethiopia kwa mabao 2-0 na kufanikiwa kusonga mbele pamoja na Burkina Faso katika Kundi na kuziacha Ethiopia pamoja na mabingwa watetezi wa michuano hiyo kuyaaga mashindano hayo. Nigeria imeshiriki Afcon mara 17 na kufanikiwa kuvuka hatua ya makundi mara 15 na sasa nchi hiyo itakwaana na Ivory Coast timu ambayo inapewa nafasi kubwa ya kunyakuwa taji la michuano hiyo. Pamoja na Ivory Coast kupewa nafasi kubwa lakini kocha Nigeria Steven Keshi amesema ameandaa mbinu madhubuti ya kupambana na wapinzani wao ili kuhakikisha wanasonga mbele kwenye michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment