Tuesday, January 29, 2013

MESSI KUSAINI MKATABA BARCELONA.

RAIS wa klabu ya Barcelona, Sandro Rosell amesema kuwa mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Lionel Messi anatarajiwa kuongeza mkataba wiki ijayo. Mkataba huo mpya ambao Messi anatarajiwa kusaini utamuweka katika klabu hiyo mpaka 2018 lakini Rosell alibainisha kuwa hakuna klabu yoyote iliyokuja kutaka kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Argentina. Rosell amesema klabu haijapokea maombi yoyote ya mchezaji huyo kutoka vilabu vingine na ana uhakika kama wapo waliomfuata lazima atakuwa amewakatalia. Messi mwenye umri wa miaka 25 anakuwa mchezaji wa tatu ndani ya wiki moja kukubali kusaini mkataba mpya kufuatia habari kuwa Carles Puyol na Xavi Hernandez nao kukubali kuongeza mikataba yao na Rosell ana uhakika golikipa Voctor Valdes naye atafuata nyayo hizo.

No comments:

Post a Comment