Thursday, January 31, 2013

SAMBA AFAULU VIPIMO VYA AFYA QPR.

KLABU ya Queens Park Rangers inakaribia kukamilisha uhamisho wa beki Christopher Samba kutoka klabu ya Anzhi Makhachkala baada ya kufikia makubaliano na mchezaji huyo kufaulu vipimo. Beki huyo wa zamani wa Blackburn mwenye umri wa miaka 28 amesajili kwa ada ya paundi milioni 12.5 ambapo atakuwa akipokea kitita cha paundi 100,000 kwa wiki ikiwemo posho na mambo mengine. Nyota huyo alithibitisha kufanyiwa vipimo vya afya jijini London katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter jana. Mbali na Samba lakini pia meneja wa QPR Harry Redknapp yuko mbioni kumfukuzia mshambuliaji wa klabu ya Stoke City Peter Crouch.

No comments:

Post a Comment