Thursday, January 31, 2013

KAGAWA AITWA TENA JAPAN.

KIUNGO nyota wa klabu ya Manchester United, Shinji Kagawa ameitwa tena katika kikosi cha timu ya taifa ya Japan kitakachocheza mchezo wa kirafiki na Latvia Jumatano ijayo baada ya kupona na kurejea katika kiwango. Kagawa alikosa baadhi ya michezo ya nchi yake ukiwemo mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia ambao walipata ushindi mwembamba wa mabao 2-1 dhidi ya Oman Novemba mwaka jana kwasababu majeraha ya mguu aliyopata wakati anaichezea United. Kagawa alirejea katika kikosi cha United Desemba baada ya kupona na ameonyesha kurejea katika kiwango chake wakati timu yake hiyo ikiongoza Ligi Kuu nchini Uingereza kwa alama saba zaidi ya mahasimu wao Manchester City wanaoshika nafasi ya pili. Kocha wa Japan Alberto Zaccheroni amesema amekuwa akimfuatilia nyota huyo katika mechi alizocheza karibuni na ameshawishika kumuita tena kuimarisha kikosi chake baada ya kurejea katika kiwango chake.

No comments:

Post a Comment