Saturday, January 26, 2013

WENGER AMTABIRIA UNAHODHA WILSHERE.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger anaamini kuwa kiungo wake nyota Jack Wilshere siku moja atakuwa nahodha wa timu hiyo pamoja na timu yake ya taifa ya Uingereza. Nyota huyo anatarajiwa kukabidhiwa unahodha katika kikosi cha timu hiyo baadae leo ambacho kitacheza mechi ya Kombe la FA dhidi ya Brighton baada ya Wenger kuamua kuwapumzisha Mikel Arteta na Thomas Vermaelen. Wenger amesema Wilshere ni mchezaji wa kiwango cha juu na mwenye uchu wa kupata ushindi kitu ambacho anatakiwa awe nacho kiongozi wa timu ili kuwahamasisha wenzake. Kocha aliendelea kusema kuwa kwa maoni yake nyota huyo anaweza kuwa nahodha mzuri wa Uingereza katika siku za baadae lakini alikataa kuingia ndani zaidi kwa kudai kuwa swali hilo anayeweza kulijibu vizuri ni kocha wa nchi hiyo Roy Hodgson.

No comments:

Post a Comment