Saturday, January 26, 2013

NIGERIA ITASONGA MBELE - OBI MIKEL.

KIUNGO wa kimataifa wa Nigeria, John Obi Mikel anaamini kuwa kikosi cha nchi hiyo kinachojulikana kama Super Eagles kitasonga katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika inayoendelea nchini Afrika Kusini. Mpaka sasa Super Eagles haijapata ushindi wowote katika michezo miwili kwenye michuano hiyo lakini wanaweza kusonga mbele kama wakishinda mchezo wao wa mwisho katika kundi C dhidi ya Ethiopia utakaochezwa Januari 29. Nigeria ilikuwa na nafasi ya kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele katika mchezo wao dhidi ya mabingwa watetezi Zambia lakini walishindwa kufanya hivyo baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na kufikisha alama mbili. Lakini Obi Mikel anaamini kuwa nchi hiyo itasonga mbele kwa kuhakikisha wanapata alama zote tatu katika mchezo wao wa mwisho dhidi ya Ethiopia. Nyota huyo anayecheza katika klabu ya Chelsea ya Uingereza aliwataka wachezaji wenzake kutokata tamaa baada ya kupata sare ya pili dhidi ya Zambia badala yake wanatakiwa wajipange ili kuhakikisha wanashinda mchezo wao ujao.

No comments:

Post a Comment