Saturday, January 26, 2013

FERGUSON AWAJIA JUU WANAOMPONDA KIPA WAKE.

MENEJA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amemkingia kifua golikia wake David de Gea baada ya nyota huyo wa kimataifa wa Hispania kulaumiwa kuruhusu bao la kusawazisha katika mchezo dhidi ya Tottenham Hotspurs mwishoni mwa wiki iliyopita. Wachambuzi wa soka wa luninga Alan Hansen na Gary Neville walimlaumu De Gea kwa makosa aliyofanya na kuruhusu Clint Dempsey kuisawazishia timu yake bao lakini Ferguson amesema hatilii maanani habari hizo. Ferguson amesema bado anamwamini De Gea kuwa golikipa wake namba moja na maneno ya watangazaji hao hayawezi kumbadilisha anavyofikiria. Katika mchezo huo United ambao ndio vinara wa Ligi Kuu nchini Uingereza ililazimishwa sare ya bao 1-1 na Tottenham bao ambalo lilisawazishwa katika dakika za lala salama.

No comments:

Post a Comment