Saturday, January 26, 2013

BEBETO KUKABIDHIWA TIMU YA VIJANA.

SHIRIKISHO la Soka nchini Brazil linajipanga kumteua mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa nchi hiyo, Bebeto kuwa kocha wa timu ya vijana chini ya miaka 20 itakayoshiriki katika michuano ya Amerika Kusini. Akihojiwa kuhusu suala hilo Bebeto amesema kuwa matokeo mabovu katika siku za karibuni yamechangia mabadiliko hayo katika timu za vijana kwakuwa ndio msingi wa kupata timu nzuri ambayo itapambana kuhakikisha wanabakisha nyumbani Kombe la Dunia 2014. Shirikisho hilo limedai kuwa nyota huyo ambaye anakumbukwa kwa aina ya ushangiliaji wake akiwa kama amempakata mtoto katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 1994 iliyofanyika Marekani atateuliwa rasmi kushika nafasi hiyo wiki ijayo. Hatahivyo wadau wa soka nchini humo wamedai kuwa Bebeto ana uwezo mdogo katika kufundisha akiwa amewahi kufundisha klabu moja ya Amerika iliyopo jijini Rio de Janeiro mwaka 2010.

No comments:

Post a Comment