Saturday, January 26, 2013

EURO 2020 KUCHEZWA KATIKA MIJI 13 TOFAUTI.

SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya-UEFA limetangaza kuwa michuano ya Ulaya 2020 itaandaliwa katika nchi 13 huku nusu fainali na fainali za michuano hiyo zitachezwa katika uwanja mmoja. Katibu Mkuu wa UEFA Gianni Infantino amesema hakuna uwanja zaidi ya mmoja utakaotumika katika nchi ambayo itapewa nafasi kuandaa mechi, katika timu 24 zinazoshiriki michuano hiyo na viwnaja hivyo vitachaguliwa Septemba mwaka 2014. UEFA walipiga kura Desemba mwaka jana kuandaa michuano hiyo katika miji tofauti kuzunguka bara hilo kuliko ilivyokuwa kawaida ambapo michuano hiyo imekuwa ikiandaliwa na nchi moja au mbili. Shirikisho limedai kuwa kufanya hivyo kutasaidia nchi ndogo ambazo hazitaweza kuzihudumia nchi 24 zinazoshiriki michuano hiyo kupata uhondo kwa kuandaa mojawapo ya mechi. Rais wa UEFA Michel Platini amesema uwanja utakaotumika kwa ajili ya mechi za nusu fainali na fainali unatakiwa kuwa na uwezo wa kuingiza mashabiki 70,000 na mashabiki 60,000 kwa viwanja vya robo fainali huku hatua ya makundi ambayo itakuwa na mechi 16 viwanja vyake vinatakiwa kuwa na uwezo wa kuingiza mashabiki 50,000.

No comments:

Post a Comment