Thursday, February 28, 2013

ARSENAL KUMTENGENEZEA BERGKAMP MWANASESERE.

KLABU ya Arsenal imebainisha kuwa ina mpango wa kumuenzi mshambuliaji nyota wa zamani wa klabu hiyo Dennis Bergkamp kwa kujenga sanamu lake nje ya Uwanja wa Emirates. Bergkamp atakuwa anafuata nyayo za wachezaji wenzake wa zamani Thierry Henry na Tony Adams pamoja na meneja nguli wa klabu hiyo Herber Chapman ambao tayari sanamu zao zenye rangi ya fedha ziko nje ya klabu hiyo yenye maskani yake kaskazini mwa jiji la London. Klabu hiyo ililazimika kuthibitisha mpango wake huo baada ya umbo la sanamu la Bergkamp kuonekana katika mtandao. Akihojiwa kuhusu mpango huo Bergkamp amesema ni heshima kubwa kwake na ana jivunia kwasababu kila mtu anajua kiasi gani anaipenda klabu hiyo na alikuwa na wakati mzuri kipindi chote alichocheza hapo. Katika kipindi chake akiwa klabuni hapo Bergkamp alifunga mabao 120 na kushinda mataji matatu ya Ligi Kuu na mengine manne ya Kombe la FA katika kipindi cha miaka 11 ambayo ameitumikia klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment