Thursday, February 28, 2013

BADO TUNA UCHU WA KUICHAPA TENA BARCELONA - ARBELOA.

BEKI wa klabu ya Real Madrid, Alvaro Arbeloa amesema timu yake imepania mchezo wa La Liga dhidi ya mahasimu wao Barcelona kuliko mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester United utakaochezwa Jumanne ijayo. Madrid walifanikiwa kuwafunga Barcelona nyumbani kwao Camp Nou kwa ushindi wa kihistoria kwa mahasimu hao wa mabao mabao 3-1 na kutinga fainali ya michuano ya Kombe la Mfalme. Barcelona mwishoni mwa wiki hii watasafiri kuelekea Santiago Bernabeu kwa ajili ya mchezo mwingine wa ligi dhidi ya Madrid ambapo utakuwa kama mchezo wa kulipiza kisasi baada ya kufungwa. Arbeloa amesema wataanza kufikiria mchezo dhidi ya United Jumapili baada ya kuhakikisha wamepata matokeo mengine mazuri dhidi ya Barcelona kama walivyofanya katika mchezo wa kwanza.

No comments:

Post a Comment