Thursday, February 28, 2013

RENARD KUSAKA VIPAJI NCHI NZIMA.

KOCHA mkuu wa timu ya taifa ya Zambia Herve Renard na benchi lake la ufundi wako katika ziara ya kuzunguka nchi nzima kutafuta wachezaji wenye vipaji ambao wataweza kujuishwa katika kikosi cha nchi hiyo ambacho kitashiriki michuano ya Challenge ya Cosafa na ile ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani-CHAN itakayofanyika Afrika Kusini 2014. Ziara ya kutafuta wachezaji hao ilianza wiki kadhaa nyuma katika mikoa yote 10 ya nchi hiyo ambayo wameigawanya katika kanda tano ili kuifanya kazi hiyo kuwa rahisi zaidi. Kazi kubwa ya benchi la ufundi litakuwa ni kutafuta wachezaji katika mikoa yote hiyo na baadae kuwapeleka katika kanda zilizoteuliwa kwa ajili ya usaili ambapo kila kanda itakuwa na wachezaji wapatao 44. Kanda zilizoteuliwa ni Ndola ambayo usaili wake utakuwa Machi mosi na 2 mwaka huu huku nyingine zilikiwa ni Kabwe, Lusaka, Livingstone na Chipata.

No comments:

Post a Comment