Tuesday, February 26, 2013

ARSENAL YATANGAZA FAIDA YA PAUNDI MILIONI 17 KATIKA KIPINDI CHA MIEZI SITA.

KLABU ya Arsenal imetangaza faida bila kutozwa ushuru kiasi cha paundi milioni 17 kwa kipindi cha miezi sita iliyoishia Novemba 30 kiasi hicho kikiwa kimepungua ukilinganisha kiasi cha paundi milioni 49 walichopata katika mwaka 2011. Katika taarifa yake iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo imesema kuwa kiasi cha paundi milioni 40.9 zilitumika kuwwasajili wachezaji Lukas Podolski, Santi Cazorla na Oliver Giroud na pia kuongeza mikataba kwa wachezaji Theo Walcott na Jack Wilshere. Mauzo ya mchezaji yalifikia kiasi cha paundi milioni 42.5 wakati mauzo ya tiketi yameshuka kutoka paundi milioni 113.5 mpaka paundi milioni 106 ikiwa ni matokeo ya kucheza michezo michache nyumbani kulinganisha na miaka iliyopita. Faida ya miezi sita ya Novemba mwaka 2011 pia ilinajumisha mauzo ya wachezaji Cesc Fabregas, Samir Nasri na Gael Clichy. Mwenyekiti wa klabu hiyo, Peter Hill-Wood amesema uwezo wao kushindana katika kiwango cha juu kwenye ligi ya nyumbani na Ulaya kunachagizwa kwa kiasi kikubwa na hali ya uchumi ambayo inaipa klabu nguvu na kujitegemea. Hata hivyo mashabiki wa Arsenal wamekuja juu baada ya timu hiyo kushindwa kunyakuwa taji lolote toka mwaka 2005 na kumtaka Wenger kutoa pesa zaidi kwa ajili ya kununua wachezaji wenye ubora kuziba pengo la Fabregas na Robin van Persie.

No comments:

Post a Comment