Friday, February 22, 2013

MUAMBA KUKABIDHI KOMBE LA LIGI.

NYOTA wa zamani wa klabu ya Bolton Wanderers, Fabrice Muamba anatarajiwa kukabidhi Kombe la Ligi kwa nahodha wa timu ambayo itashinda katika mchezo wa fainali kati ya Bradford City na Swansea City katika Uwanja wa Wembley baadae leo. Muamba atakuwa mgeni rasmi katika mchezo huo na pia atatizama mechi hiyo upande maalumu kwa ajili ya wageni mashuhuri na kutambulishwa kwa pande zote mbili kabla ya mchezo huo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 alilazimika kustaafu soka kabla ya muda baada ya kuzimia uwanjani wakati akichezea klabu ya Bolton kwenye robo fainali ya Kombe la FA dhidi ya Tottenham Hotspurs Machi mwaka jana. Muamba ambaye alikuwa akicheza nafasi ya kiungo moyo wake ulisimama kwa dakika 78 lakini kwasababu ya matibabu aliyopatiwa uwanjani wakati akianguka alifanikiwa kuzinduka na baadae kupona kabisa.

No comments:

Post a Comment