Friday, February 22, 2013

REAL MADRID WAINGIA MKATABA NA NIVEA.

KLABU ya Real Madrid na kampuni ya Beiersdorf AG wameingia mkataba wa udhamini kwa ajili ya kuitangaza klabu na kampuni hiyo ya vipodozi inayotengeneza mafuta ya Nivea kwa ajili ya kulinda ngozi. Rais wa Madrid Florentino Perez na ofisa mkuu wa kampuni hiyo walifikia makubaliano kwa mkataba ambao utaishia katikamsimu wa mwaka 2015-2016 katika makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo katika Uwanja wa Santiago Bernabeu jana. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya makubaliano hayo Pereza amesema Nivea itakuwa ni mojawapo wa wadhamini wao na watakuwa pamoja katika kuhakikisha wanajimiza malengo yao pamoja na changamoto zingine zitakazojitokeza. Kampeni mpya ya matangazo ya Nivea itawashirikisha nyota kadhaa wa klabu hiyo akiwemo Sergio Ramos, Marcelo, Gonzalo Higuain na Alvaro Arbeloa.

No comments:

Post a Comment