Friday, February 22, 2013

SHABIKI WA TOTTENHAM AHADITHIA WALIPOVAMIWA NA WAHUNI HUKO LYON.

MSHABIKI wa klabu ya Tottenham Hotspurs amedai alikuwa akihofia maisha yake wakati yeye na mwanae walipovamiwa na kikundi cha wahuni jijini Lyon, Ufaransa. Paul Eccles mwenye umri wa miaka 51 alipigwa ngumi na mateke katika tukio hilo na watu wapatao 20 ambao walivamia bar iliyokuwa na mashabiki wa Tottenham waliokwenda kuishangilia timu yao katika mchezo wa Europa League. Eccles ni mmoja kati ya mashabiki watatu ambao walikimbizwa hospitalia kwa ajili ya matibabu baada ya tukio hilo. Shabiki huyo amesema lilikuwa ni jambo la kuogopesha wakati yuko amelala chini huku akipigwa alikuwa akitegemea kuchomwa mgongoni kisu muda wowote na wahuni hao. Eccles anadai kuwa pamoja na kipigo hicho hawezi kuacha kusafiri kuishangilia timu yake ambapo sasa anapanga kwenda Italia kuishangilia timu hiyo ikicheza na Inter Milan mwezi ujao kama afya yake itamruhusu.

No comments:

Post a Comment