Friday, February 22, 2013

WENGER APANIA KUVUNJA BENKI MAJIRA KIANGAZI.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amedai kuwa anaweza kutoa kitita cha paundi milioni 80 kwa ajili ya kumsajili Radamel Falcao wakati timu hiyo ikijiandaa kubadilisha mfumo wake wa matumizi. Wenger ambaye yuko katika shinikizo kubwa kutoka kwa mashabiki baada ya kikosi chake kuchapwa na Bayern Munich katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya anatarajiwa kukabidhiwa kitita kikubwa kwa ajili ya usajili katika kipindi cha majira ya kiangazi. Wenger amedai kuwa wanaweza kufikia kiasi cha paundi milioni 40 kama Atletico Madrid itakuwa kumuuza Falcao na pia wanaweza kufikia kiwango cha mshahara atakachohitaji nyota huyo wa kimataifa kutoka Colombia. Kocha huyo anadai kuwa alikuwa na kitita cha kutosha katika kipindi cha dirisha dogo la usajili la Januari lakini alishindwa kusajili baada ya kukosa aina ya mchezaji ambaye anamuhitaji.

No comments:

Post a Comment