Friday, February 22, 2013

CASILLAS KUREJEA BAADA YA WIKI NNE.

GOLIKIPA wa kimataifa wa Hispania na klabu ya Real Madrid, Iker Casillas amesema anatarajia kurejea tena uwanjani baada ya wiki nne zijazo. Casillas alivunjika kidole gumba katika mchezo wa Kombe la Mfalme dhidi ya Valencia Januari mwaka huu na baadae kufanyiwa upasuaji ili kurekebisha tatizo hilo. Upasuaji huo umepelekea nahodha huyo wa Madrid kuwekewa skrubu mbili katika kidole gumba chake zoe zilikiwa na urefu wa milimita 17 na upana wa milimita mbili. Casillas amesema anategemea kurejea uwanjani baada ya mwezi mmoja baada ya madaktari kumhakikishia hivyo na tayari ameanza kufanya mazoezi mepesi na anaweza kuchezesha kidole chae kilichofanyiwa upasuaji. Hatahivyo, Casillas atatakiwa kupigania nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza baada ya kupona kidole chake baada ya Jose Mourinho kumuengua katika kikosi chake kutokana na majeruhi huku kukiwa na ujio wa golikipa mpya Diego Lopez kutoka Sevilla.

No comments:

Post a Comment