Wednesday, February 27, 2013

FRINGS ATUNDIKA DARUGA.

MCHEZAJI wa zamani wa kimataifa wa Ujerumani na nahodha wa klabu ya Toronto FC Torsten Frings ametangaza kustaafu soka akidai kuwa hawezi kurejea katika kiwango chake kufuatia kukoa msimu kutokana na kufanyiwa upasuaji wa nyonga. Frings ambaye ameichezea timu ya taifa ya Ujerumani mechi 79 na kucheza fainali mbili za Kombe la Dunia zikiwemo za mwaka 2002, ameitumikia Toronto kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu baada ya kucheza kwa mafanikio katika vilabu vya Bayern Munich, Werder Bremen na Borussia Dortmund. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 36 ndio alikuwa akilipwa zaidi katika klabu hiyo akichukua kitita cha dola milioni 2.43 lakini imebidi akatishe soka lake huko Marekani kutokana na majeruhi. Katika taarifa yake Frings amesema amgundua kuwa kupona kwake kutachukua muda mrefu kuliko alivyotegemea nay eye siku zote anataka kucheza kwa kiwango cha juu ili kuisasidia timu yake ndio maana ameamua kukaa pembeni ili aendelee kujiuguza taratibu.

No comments:

Post a Comment