Wednesday, February 27, 2013

TUNATAKIWA KUONGEZA BIDII ZAIDI - FABREGAS.

NYOTA wa zamani wa klabu ya Arsenal, Cesc Fabregas anadhani wachezaji wa timu yake ya Barcelona wanatakiwa kuongeza bidii zaidi uwanjani na kusahau machungu ya kufungwa waliyopata jana. Fabregas alisisitiza kwamba timu hiyo inatakiwa kujifunza kutokana na kipigo walichopata cha mabao 3-1 dhidi ya mahasimu wao Real Madrid jana usiku katika nusu fainali ya Kombe la Mfalme. Katika nusu fainali ya kwanza Barcelona walifanikiwa kupata matokeo ya sare ya bao 1-1 nyumbani kwa Madrid lakini walishindwa kutamba katika mchezo wao wa marudiano uliofanyka nyumbani kwao kwa kukubali kipigo hicho. Fabregas amesema wanatakiwa kujifunza kutokana na kipigo hicho ili kujipanga kuhakikisha wanashinda mchezo wao wa La Liga dhidi ya mahasimu wao hao Jumamosi kwani bado wana mataji ya kushindania. Barcelona katika mechi za karibuni imeonyesha kupunguza kasi yake waliyoanza nayo baada ya pia kukubali kipigo cha mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya AC Milan.

No comments:

Post a Comment