Tuesday, February 26, 2013

INTER YATOZWA FAINI.

KAMATI ya nidhamu ya Ligi Kuu nchini Italia maarufu kama Serie A limeitoza faini ya euro 50,000 klabu ya Inter Milan baada ya mashabiki wake kukutwa na hatia ya kumfanyia vitendo vya kibaguzi mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo Mario Balotelli. Tukio lilitokea wakati Balotelli akiichezea kabla yake mpya ya AC Milan katika mchezo dhidi ya Inter ambao ulimalizika kwa sare ya kufungana bao 1-1. Mashabiki wa Inter walikuwa wakipeperusha maganda ya ndizi katika mchezo huo lakini baadhi wachambuzi walidai pengine tukio hilo halikumlenga nyota huyo ambaye ameitumikia klabu hiyo kwa miaka minne. Balotelli ambaye ametokea Manchester City kabla ya kwenda AC Milan naye pia metozwa euro 10,000 kwa kuwaonyesha ishara ya matusi mashabiki hao. 

No comments:

Post a Comment