Tuesday, February 26, 2013

SHIRIKISHO LA SOKA LIBYA LAFANYA UCHAGUZI WA KWANZA TOKA MWAKA 1962.

SHIRIKISHO la Soka nchini Libya, FLF Jumatatu limemteua rais wa kwanza toka kuanzishwa kwa shirikisho hilo mwaka 1962. Anouer al-Tachan ndio jina lililoibuka kidedea katika uchaguzi huo ambao ulihudhuriwa na vilabu mbalimbali nchini humo. Katika mfumo wa zamani shirikisho hilo lilikuwa likimilikiwa na familia ya rais wa zamani wan chi hiyo Muammar Gaddafi haswa watoto wa kiume wa rais huyo Saadi na Mohammed. Mfumo mpya katika shirikisho hilo hivi sasa una wajumbe wakuchaguliwa wapatao 12 ambao kazi yao kubwa itakuwa kuratibu na kuweka mfumo mzuri wa uongozi katika kipindi cha mwaka mmoja watakachotawala. Ligi Kuu nchini humo bado haijachezwa toka kuanguka utawala wa zamani mwaka 2011 kutokana na harakati za kuhakikisha usalama unaimarika kwanza kabla ya kuanza.

No comments:

Post a Comment