Tuesday, February 26, 2013

BARCELONA BADO YAMNYATIA NEYMAR.

MAKAMU wa rais wa klabu ya Barcelona, Josep Bartomeu amebainisha kuwa klabu hiyo iko tayari kuanza mbio za kumsajili mshambuliaji nyota wa klabu ya Santos, Neymar mara watakapopata ishara kwamba nyota huyo yuko tayari kuondoka. Mshambuliaji huyo nyota wa kimataifa kutoka Brazil, anaendelea kuhusishwa na kuhamia vilabu vya Ulaya lakini mwenyewe amesisitiza mara kwa mara kuwa hana haraka ya kuondoka nchini kwake kabla ya Kombe la Dunia 2014 ambalo litafanyika katika ardhi yao. Hatahivyo pamoja na kauli ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 21 lakini klabu hiyo imeendelea kumfuatilia nyendo zake na wako tayari kumchukua wakati atakapoamua kuondoka Santos. Mkataba wa Neymar unamalizika baada ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014.

No comments:

Post a Comment