Tuesday, February 26, 2013

ETO'O APOKELEWA KISHUJAA GUINEA.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Cameroon, Samuel Eto’o amepokelewa kishujaa na maelfu ya mashabiki jijini Conakry nchini Guinea kabla ya kukutana na rais wan chi hiyo Alpha Conde na baadhi ya mawaziri ka maongezi binafsi. Eto’o ambaye amewahi kunyakuwa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika mara nne baadae alitembelea uwanja mpya wa Nongo wenye uwezo wa kuingiza watu 50,000 wilaya ya kaskazini mwa mji huo. Wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika makao makuu ya Shirikisho la Soka la Guinea, Eto’o alieleza sababu za yeye kutembelea nchi hiyo kuwa anataka kufanya mazungumzo kwa ajili ya shule ya soka kwa vijana wan chi hiyo. Nyota huyo ambaye amewahi kucheza katika vilabu vya Barcelona, Inter Milan na sasa Anzi Makhachkala ya Urusi tayari ameshafungua shule za soka nchini kwake Cameroon na Gabon ambapo wanafunzi wanasoma bure. Matunda ya shule hizo tayari yameshaanza kuonekana baada ya mshambuliaji mwenye umri wa miaka 16 Fabrice Olinga kutoka Cameroon kunyakuliwa na klabu ya Malaga inayoshiriki Ligi Kuu nchini Hispania akitokea katika shule hizo.

No comments:

Post a Comment