Tuesday, February 26, 2013

MCLAREN ATIMULIWA FC TWENTE.

KOCHA wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza, Steve McClaren amejiuzulu wadhfa wake wa kuinoa klabu ya FC Twente ya Uholanzi siku moja baada ya kufanya mazungumzo na mwenyekiti wa klabu hiyo Joop Munsterman. Klabu hiyo haijashinda mchezo wowote wa ligi toka Desemba 21 na wapo katika nafasi ya tano katika msimamo wa ligi wakiwa nyuma kwa ya PSV Eindhoven wanaoongoza ligi kwa alama sita. MacClaren amesema kuwa wamekubaliana na uongozi kwa lazima aondoke kwa manufaa ya klabu na anaondoka akiwa mtu anayejivunia baada ya kuiwezesha klabu hiyo kunyakuwa taji la ligi mwaka 2010. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 51 alijiunga na Twente baada ya kutimuliwa kibarua cha kuinoa Uingereza Novemba mwaka 2007 kufuatia nchi hiyo kushindwa kufuzu michuano ya Kombe la Ulaya mwaka 2008.

No comments:

Post a Comment