Thursday, February 28, 2013

LIGI KUU NCHINI UINGEREZA KUTUMIA GOAL LINE TECHNOLOGY MSIMU UJAO.

LIGI kuu nchini Uingereza inatarajiwa kuanza kutumia mfumo wa teknologia ya kompyuta katika mstari wa goli wakati msimu mpya wa ligi hiyo 2013-2014. Mfumo huo ulifanyiwa majaribio na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia iliyofanyika Desemba mwaka jana na tayari viongozi wa ligi hiyo wameshaanza mazungumzo na kampuni zilizopewa dhamana ya kufunga vifaa hivyo. Msemaji wa ligi hiyo Dan Johnson amesema mara msimu ujao utakapoanza klabu zote zitalazimika kuwa na mfumo huo zikiwemo klabu ambazo zitakuwa zimepanda daraja. Mifumo miwili ya Hawkeye na GoalRef ambayo ndio imepitishwa na FIFA yote ilitumika katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia kwa mafanikio. 

No comments:

Post a Comment