Thursday, February 28, 2013

DJOKOVIC, FEDERER WATINGA NUSU FAINALI DUBAI.

WACHEZAJI nyota wa mchezo wa tenisi Novak Djokovic na Roger Federer wameendelea kung’ara katika michuano ya Dubai baada ya wote kutinga hatua ya nusu fainali. Djokovic ambaye anashika namba moja katika orodha za ubora duniani alifanikiwa kutinga hatua hiyo baada ya kumfunga Andreas Seppi wa Italia kwa 6-0 6-3 na sasa anatarajiwa kukutana na Juan Martin del Porto wa Argentina. Federer anayeshika namba mbili katika orodha hizo anaye alimsambaratisha bila huruma Nikolay Davydenko kwa 6-2 6-2 na sasa nyota huyo raia wa Switzerland atakutana na Tomas Berdych wa Jamhuri ya Czech. Berdych alitinga hatua hiyo kwa kumfunga Dmitry Tursunov wa Urusi kwa 6-3 6-2 wakati Del Potro yeye alimfunga Daniel Brands wa Ujerumani kwa 6-4 6-2 na kuhakikisha nyota wanaoshika nafasi nne za juu kukutana katika hatua ya nusu fainali.

No comments:

Post a Comment