Thursday, February 28, 2013

WAMBURA AMSHUKIA TENGA.

KATIBU wa zamani wa Shirikisho la Soka nchini-TFF au FAT kama ilivyokuwa ikijulikana kipindi hicho, Michael Wambura amemshukia rais wa shirikisho akidai anapaswa kulaumiwa kama Tanzania ikifungiwa na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA. Kauli hiyo ya Wambura imekuja baada ya serikali kufuta katiba mpya na kuiamuru TFF itumie katiba ya zamani ya mwaka 2006 katika kufanya mchakato wa uchaguzi. Wambura amesema TFF kama taasisi nyingine inapaswa kufanya kazi zake kwa kufuata misingi na sheria za nchi hivyo ni jukumu lao kuhakikisha wanatekeleza agizo hilo la serikali. Wambura amesema kama FIFA ikiifungia Tanzania kushiriki michuano ya kimataifa kutokana na kauli hiyo ya Serikali lawama zote anapaswa kupewa Tenga kwani yeye ndio chanzo cha mgogoro huu unaondelea hivi sasa. 

No comments:

Post a Comment