Thursday, February 28, 2013

UNITED KUFANYA ZIARA THAILAND.

KLABU ya Manchester United imetangaza kuwa itafanya ziara nchini Thailand kwa ajili maandalizi ya msimu mpya wa 2013-2014 wa Ligi Kuu nchini Uingereza. United ambao kwasasa wanaongoza msimamo wa ligi hiyo wanatarajiwa kuiva Singha All Star jijini Bangkok Julai 13 mchezo ambao utafanyika katika Uwanja wa Rajamangala. Klabu tayari imeshafanya ziara mara nne katika nchi hiyo lakini hawajacheza mechi yoyote kwa kipindi cha miaka 12 iliyopita. Klabu hiyo pia katika maandalizi yake ya msimu ujao itacheza mechi za kujipima nguvu katika miji ya Sydney, Tokyo, Osaka na Hong Kong.

No comments:

Post a Comment