Wednesday, February 20, 2013

MOURINHO NI MKALI ZAIDI - DEL BOSQUE.

KOCHA wa timu ya taifa ya Hispania, Vicente Del Bosque ameweka wazi ufananisho kati yake na kocha wa klabu ya Reala Madrid, Jose Mourinho na kudai kuwa mreno huyo huwa anakuwa mkali zaidi wakati akifundisha. Del Bosque ambaye ameiwezesha nchi hiyo kunyakuwa Kombe la Dunia 2010 pamoja na kutetea taji lao la Ulaya mwaka jana anadai huwa anakuwa mtulivu zaidi wakati akifundisha kuliko mwenzake Mourinho. Madrid ambao ni mabingwa watetezi wa La Liga kwasasa wapo katika nafasi ya tatu mwa msimamo wa ligi hiyo wakipishana kwa alama 16 na mahasimu wao Barcelona ambao wameshikilia usukani kitu ambacho watu wameanza kuhoji juu ya ufundishaji wa kocha huyo. Del Bosque mwenye umri wa miaka 62 aliendelea kudai kuwa kuna vitu vingi vya kuangalia kama sifa na utashi wa mtu ndio maana anajiona mtulivu zaidi ya Mourinho.

No comments:

Post a Comment