Friday, February 22, 2013

SIJAFIKIRIA KUACHIA NGAZI HATA SEKUNDE MOJA - WENGER.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema hakuna hata sekunde moja aliyofikiria kuachia kibarua cha kuinoa klabu hiyo wiki hii. Kauli hiyo imekuja kutokana na nafasi finyu waliyonayo Arsenal kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-1 katika mchezo wa kwanza na kufuatiwa kutolewa pia katika mzunguko wa tano wa Kombe la FA na Blackburn Rovers. Wenger amedai kuwa wanatakiwa kuwa na umoja na nguvu na kuvurugwa na watu ambao wanakuwa na mawazo hasi baada ya timu kufanya vibaya katika mchezo mmoja. Kocha huyo amekuwa akipewa wakati mgumu na mashabiki wa klabu hiyo wengi wao wakitaka aachie nafasi hiyo baada ya kushindwa kuipa taji lolote Arsenal toka mwaka 2005 wakati walipoifunga Manchester United kwa matuta kwenye Kombe la FA. Lakini wakati akiulizwa swali hilo katika mkutano na waandishi wa habari kabla ya mchezo wao na Aston Villa utakaochezwa kesho Wenger amesema hajafikiria kujiuzulu wadhifa wake huo hata kwa sekunde moja kwani ana mkataba mpaka mwaka 2014 ndipo hatma yake itakapojulikana.

No comments:

Post a Comment