Sunday, March 31, 2013

FIFA YAIONYA AFRIKA KUSINI.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limeiandikia barua serikali ya Afrika Kusini kuwaonya kufanya uchunguzi wa kimahakama juu ya kashfa ya upangaji matokeo wakidai kuwa suala hilo ni bora likashughulikiwa na Chama cha Soka cha nchi hiyo-SAFA. Mechi kadhaa za Afrika Kusini walizocheza kabla ya michuano ya Kombe la Dunia 2010 zimegundulika kwamba zilipangwa na kupelekea baadhi ya viongozi wa juu wa SAFA kusimamishwa akiwemo rais wake Kirsten Nematandani. Shirikisho la Michezo nchini humo pamoja na Kamai ya Olimpiki wamependekeza kufanyika uchunguzi wa kimahakama lakini FIFA waliwaonya juu ya madhara yanayoweza kuwakuta kama serikali itaonekana kuingilia masuala ya soka. Waziri wa Michezo wa Afrika Kusini, Fikile Mbalula aliviambia vyombo vya habari vya nchi hiyo kuwa atasafiri kwenda makao makuu ya FIFA jijini Zurich wiki ijayo kwa ajili kuzungumzia suala hilo.

No comments:

Post a Comment