Thursday, March 28, 2013

UWANJA WA OLIMPIKI BRAZIL WAFUNGWA.

UWANJA ambao umepangwa kutumika kwa ajili ya michuano ya Olimpiki 2016 itakayofanyika nchini Brazil umefungwa kwa muda usiojulikana kwasababu ya matatizo ya kimiundo mbinu katika paa lake. Uwanja huo uitwao Joao Havelange lilikiwa ni jina la rais wa zamani wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA uliopo jijini Rio de Janeiro ulijengwa miaka sita iliyopita. Ndio uwanja uliokuwa ukitumika katika mechi mbalimbali za soka jijini humo wakati Uwanja wa Maricana ukiwa umefungwa kwa matengenezo kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Mamlaka zinazohusika pia zilikiri kuchelewa kwa ukarabati wa Maricana na tatizo la fedha katika matengenezo ya viwnaja vingine ambavyo vitatumika kwa ajili ya mechi za ufunguzi za Kombe la Dunia. Meya wa jiji hilo Eduardo Paes alithibisha kuufunga uwanja huo kwa matengenezo baada ya kupokea taarifa za kiufundi kuwa paa lake haliko salama kwa matumizi.

No comments:

Post a Comment