Wednesday, April 24, 2013

BABU YAKE VAN PERSIE AMPONGEZA MJUKUU WAKE.

BABU yake mshambuliaji nyota wa Manchester United, Robin Van Persie amempongeza mjukuu wake kwa kunyakuwa taji la Ligi Kuu nchini Uingereza na kudai kuwa amemuandalia zawadi kubwa ya busu wakati atakapokutana na nyota huyo mwezi ujao. Mzee huyo aitwaye Wim Camp alikuwa akitizama katika luninga akiwa nyumbani kwake Prinksenbeek, Breda nchini Uholanzi wakati mwanae alipofunga mabao yote matatu katika ushindi uliowahakikishia ubingwa wa ligi hiyo huku wakiwa wamebakiwa na michezo sita mokononi. Camp mwenye umri wa miaka 92 bado hajazungumza na mjukuu wake toka wafanikiwe kunyakuwa taji hilo lakini amedai anasubiri kwa hamu ili aweze kumpa pongezi zake kipindi watakapokutana. Mzee huyo amedai anatarajia kumtembelea mjukuu wake Mei 4 wakati ambapo Manchester United watakwaana na Chelsea ingawa amedai kuwa mechi hiyo haitakuwa muhimu sana lakini lazima amkumbatie na kumpiga busu kwa kazi nzuri aliyofanya. 

No comments:

Post a Comment