Wednesday, April 24, 2013

MAREKANI KUMDAI ARMSTRONG FIDIA.

SERIKALI ya Marekani inataka fidia ya zaidi paundi milioni 78 baada ya kufungua mashtaka dhidi ya mwendesha baiskeli Lance Armstrong. Mwendesha baiskeli huyo mwenye umri wa miaka 41 ambaye amefungiwa anatuhumiwa kukiuka masharti ya mkataba na timu yake ya zamani na anatajwa kupata utajiri kwa njia ya udanganyifu wakati alipodanganya na kushinda mashindano ya Tour de France. Katika taarifa iliyowasilishwa mahakamani imedai kuwa watoa Huduma za Posta nchini Marekani wamekuwa wakilipa kiasi cha paundi milioni 26 kwa ajili ya udhamini wa timu ya baiskeli ya nchi hiyo kuanzia mwaka 1998 mpaka 2004. Armstrong amekiri kuwa alikuwa akitumia dawa za kuongeza nguvu katika mataji yake yote saba ya Tour de France aliyowahi kushinda.

No comments:

Post a Comment