Monday, April 22, 2013

BAHRAIN GRAND PRIX KUPEWA MIAKA MINGINE MITANO.

MMILIKI wa mashindano ya magari yanayokwenda kasi ya langalanga Bernie Ecclestone amesema atakuwa mtu mwenye furaha kama watawaongeza mkataba mwingine wa miaka mitano Bahrain Grand Prix pamoja na utata uliopo juu ya suala la usalama. Ecclestone ambaye mara nyingi amekuwa akiikosoa serikali ya Bahrain kwa kupewa dhamana na kuandaa mashindano hayo kwasababu ya kutoa nafasi kwa waandamanaji wa kisiasa. Lakini mara baada ya mashindano yaliyomalika Jana na taji kuchukuliwa na Sebastian Vettel wa Red Bull, bosi amesema watakuwa na furaha kuwapa Bahrain mkataba mpya wa miaka mitano kwani anadhani wamefanya kazi nzuri na hajaona tatizo lolote. Miaka miwili iliyopita mashindano hayo yalisogezwa mbele na baadae kusimamishwa kabisa baada ya maandamano ya kidemokrasia yasiyokoma yaliyopelekea watu 35 kufariki kutokana na vurugu hizo. Mwaka jana Bhrain iliruhusiwa kuandaa michuano hiyo baada ya Ecclestone na Chama cha Mashindano ya Langalanga-FIA kudai kuwa wamehakikishiwa kuwepo kwa usalama wa kutosha katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment