Monday, April 22, 2013

CISSE AONJA JOTO LA UBAGUZI BAADA YA KUAMUA KUTOKA NA MZUNGU.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Newcastle United, Papiss Cisse na rafiki yake wa kike wamekuwa wakitumiwa ujumbe na watu mbalimbali ambao ni wabaguzi wakipinga mahisiano yao. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Senegal mwenye umri wa miaka 27 ana mahusiano na Rachelle Graham mwenye umri wa miaka 22 ambaye ni mnyange wa mji wa Newcastle. Mnyange huyo ambaye ni mzungu alilikuwa akichangisha fedha kwa kuruka umbali wa futi 13,000 kutoka angani ili ziweze kusaidia kununulia gari la wagonjwa kwenda Senegal na wawili hao walitumiwa ujumbe wa kibaguzi katika mtandao kwa sababu ya tukio hilo. Polisi wa Newcastle wanafuatialia tukio hilo kama uhalifu wa chuki baada ya mama yake Rachelle kutoa taarifa za mtandao huo.

No comments:

Post a Comment