Monday, April 22, 2013

PFA KUMPA USHAURI NASAHA SUAREZ.

CHAMA cha Wanasoka wa Kulipwa-PFA kimesema kuwa mshambuliaji nyota wa Liverpool, Luis Suarez atapatiwa ushauri wa namna ya kuzikabili hasira zake kufuatia tukio lake la kumg’ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay tayari ameshamuomba radhi Ivanovic kwa tukio hilo alilofanya katika mchezo wa ligi baina ya timu hizo ambao uliisha kwa sare ya mabao 2-2 lakini klabu yake imeshamtoza faini na kunauwezekano mkubwa FA nao wakatoa adhabu baadae. Suarez mwenye umri wa miaka 26 alifungiwa kucheza mechi saba baada ya kufanya tukio kama hilo wakati akiwa katika klabu ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi kipindi cha nyuma ambapo alimng’ata Otman Bakkal wa PSV. Nyota huyo asiyetabirika pia alishawahi kufungiwa mechi nane katika Ligi Kuu nchini Uingereza baada ya kumfanyia vitendo vya kibaguzi Patrice Evra wa Manchester United. Ofisa Mkuu wa PFA Gordon Taylor amesema hakuna shaka juu ya kiwango bora alichonacho nyota huyo lakini inasikitisha kwa vitendo vya ambavyo amekuwa akivifanya ndio maana wameamua kumsaidia ili aweze kuzikabili hasira zake.

No comments:

Post a Comment