Wednesday, April 24, 2013

Bayern Munich VS Barcelona 4-0 (23-4-2013) Highlights

MABINGWA wa Ujerumani, Bayern Munich wamejiweka katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya fainali ya michuano ya klabu bingwa barani Ulaya baada ya kuitandika Barcelona 4-0 katika mchezo wa kwanzawa nusu fainali nchini Ujerumani. Mabao mawili ya Thomas Müller, na yale ya Mario Gomez na Arjen Robben yaliizamisha Barcelona ambayo ilikuwa na nyota wake wote wakutegemewa, akiwemo Messi ambaye alikosa michezo kadhaa kabla ya kuanzishwa usiku huu. Hii imekuwa mara ya kwanza kwa Barcelona kufungwa mabao 4-0 tangu mwaka 1997 walipofungwa na Dynamo Kiev ya Urusi mwaka 1997 kwenye hatua ya robo fainali ya michuano ya klabu bingwa barani ulaya. Bayern Munich wametoka kutawazwa kuwa mabingwa wa Ujerumani wiki chache zilizopita na iwapo watafanikiwa kuiondosha Barcelona na kutinga hatua ya fainali ya michuano ya klabu bingwa, itakuwa fainali yao ya tatu kushiriki ndani ya miaka minne. Michuano hiyo itaendelea tena leo usiku ambapo mahasimu wa Barcelona, Real Madrid watakuwa na kibarua kizito pale itakapokaribishwa katika Uwanja wa Signal-Iduna-Park kukwaana na wenyeji Borussia Dortmund kwenye mchezo unaotaajiwa kuwa mgumu na wa kusisimua.

No comments:

Post a Comment