Wednesday, April 24, 2013

RONALDINHO APEWA UNAHODHA MECHI DHIDI YA CHILE.

RONALDINHO anatarajiwa kupewa unahodha wa timu ya taifa ya Brazil katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Chile hatua ambayo itamuweka katika nafasi nzuri ya kujumuishwa katika kikosi kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Shirikisho. Kocha wa Brazil Luis Felipe Scolari ameonyesha matumaini yake kwa Ronaldinho ambaye amaewahi kunyakuwa tuzo ya mchzaji bora wa dunia mara mbili kwa kumpa unahodha kwenye mechi ya mwisho kabla hajatangaza kikosi cha michuano ya Kombe la Shirikisho. Scolari tayari amebainisha kuwa kuna uwezekano akamchukua kati ya Ronaldinho au Kaka kwa ajili ya michuano hiyo itakayofanyika June mwaka huu. Kaka atakosa mchezo dhidi ya Chile kwasababu ni wachezaji wanaocheza katika vilabu vya Brazil peke ndio waliochaguliwa kwa ajili ya mchezo huo kirafiki kitendo ambacho kinampa nafasi kubwa kama akionyesha kiwango kizuri.

No comments:

Post a Comment