Wednesday, April 24, 2013

CAVANI ATENGEWA MKATABA MNONO NA PSG.

KLABU ya Paris Saint-Germain-PSG ya Ufaransa imemtengea mkataba mnono wa euro milioni 8.5 kwa msimu mshambuliaji nyota wa Napoli ya Italia Edinson Cavani. Imeripotiwa na vyombo vua habari nchini humo kuwa mkurugenzi wa michezo wa klabu ya PSG, Leonardo ameshafanya vikao kadhaa na wakala wa nyota huyo kuzungumzia uhamisho wake kutoka Napoli ambao unakaribia kufikia kiasi cha euro milioni 63. Mbali na PSG vilabu vingine vikubwa barani Ulaya ambavyo vimeonyesha nia ya kuhitaji sahihi ya nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay ni pamoja na Real Madrid, Manchester City na Chelsea. Cavani mwenye umri wa miaka 26 ana mkataba na Napoli mpaka 2015 ambao unamuwezesha kulipwa kiasi cha euro milioni 1.4 kwa msimu.

No comments:

Post a Comment