Monday, April 29, 2013

BECKENBAUER AIONYA BAYERN.

MCHEZAJI nyota wa zamani wa Ujerumani Magharibi, Franz Beckenbauer ameionya klabu ya Bayern Munich kuwa Barcelona haitasita kutumia mbinu chafu katika mchezo wa marudiano ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano. Barcelona walibamizwa mabao 4-0 katika mchezo wa kwanza uliochezwa Allianz Arena wiki iliyopita na Beckenbauer ana wasiwasi kuwa Barcelona watatumia mbinu zote kuhakikisha wanageuza ametokeo hayo. Amesema katika mchezo huo Barcelona itatumia mbinu zote katika kitabu kujaribu kuitoa Bayern mchezoni na kama wakishindwa hawatasita kutumia mbinu chafu mradi wafanikiwe lengo lao. Lakini pamoja na yote hayo Beckenbauer hadhani kama Bayern wataifanya kazi ya Barcelona kugeuza matokeo kuwa rahisi sana kutokana na kikosi bora walichonacho hivi sasa.

No comments:

Post a Comment