Monday, April 29, 2013

WACHEZAJI NA HUGHES NDIO CHANZO CHA QPR KUSHUKA DARAJA.

MCHEZAJI mtukutu wa Queens Park Rangers-QPR ambaye anacheza kwa mkopo katika klabu ya Olympique Marseille ya Ufaransa Joey Barton amewaponda wachezaji pamoja na kocha aliyetimuliwa Mark Hughes kuwa ndio chanzo cha timu hiyo kushuka daraja msimu huu. Barton aliondoka QPR na kujiunga na Marseille mwanzoni mwa msimu lakini kiungo huyo wa zamani wa Manchester City haraka amewalaumu wachezaji wenzake na Hughes ambaye ndiye aliamua kumpeleka kwa mkopo ufaransa. Kiungo huo aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter mara baada ya QPR kuthibitika kushuka darajakwa kutoka sare ya bila ya kufungana na Reading, kuwa uamuzi wa Hughes kununua wachezaji wanaolipwa fedha nyingi kabla ya kuanza kwa msimu ndio chanzo cha timu hiyo kushuka daraja. Wachezaji wa fedha nyingi waliosajiliwa hawakuwa wakicheza kwa kujituma akimtolea mfano Jose Bosingwa ambaye alikuwa akitoka uwanjani huku akicheka wakati timu yao imeshuka daraja. Barton amesema ni aibu kuona mchezaji ambaye amekuwa akilipwa fedha nyingi anatoka uwanjani huku anacheka wakati timu imefanya vibaya hiyo inaonyesha wazi kwamba walikuwa hawajitumi ili kuhakikisha timu yao inapata matokeo mazuri.

No comments:

Post a Comment