Monday, April 29, 2013

SHAKHTAR DONETSKI WATAWADHWA MABINGWA UKRAINE KWA MARA YA NNE MFULULIZO.

KLABU ya Shakhtar Donetski imefanikiwa kunyakuwa taji la nne mfululizo la Ligi Kuu nchini Ukraine baada ya kufanikiwa kupambana wakitoka nyuma na kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya Metalist Kharkiv. Mchezaji wa Brazil Ilsinho ndio aliyekuwa shujaa wa mchezo huo baada ya kufanikiwa kuisawazishia timu yake bao katika dakika ya 84 baada ya mshambuliaji wa zamani wa Shakhtar Marco Devic kuifungia timu yake bao la kuongoza katika dakika ya 34. Mpaka sasa Shakhtar imefanikiwa kushinda jumla ya mataji nane ya ligi kwa kuziacha Metalist na Dynamo Kiev pengo la alama 15 nyuma huku kukiwa kumebakia mechi nne kabla ya msimu kumalizika. Shakhtar pia imeweka rekodi ya kushinda taji hilo kwa haraka zaidi katika historia ya Ligi Kuu nchini Ukraine.

No comments:

Post a Comment