Monday, April 29, 2013

JAY Z ASHUHUDIA ARSENAL IKITOA SARE EMIRATES.

MWIMBAJI wa kundi la Coldplay la Uingereza na rapa machachari wa Marekani Jay Z walionekana kuwa kivutio kikubwa katika mchezo kati ya Arsenal na Manchester United uliochezwa katika Uwanja wa Emirates ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1. Wawili hao walionekana katika jukwaa maalumu wakishukuhudia mtanange huo na kuonyesha mapenzi makubwa kwa Arsenal. Miaka mitatu iliyopita Jay Z alikaririwa akisema kuwa anataka kuwekeza mahela yake katika klabu hiyo ingawa alikiri kutokuwa na uzoefu wa kutosha katika sekta hiyo. Jay Z ambaye alikuwa akivutiwa na nyota wa zamani wa Arsenal Thierry Henry bado amesisitiza nia yake ya kuwekeza Arsenal akidai kuwa atakapopata nafasi atafanya hivyo kwasababu yeye ni mfanyabiashara. Arsenal inaweza kujiimarisha zaidi kiuchumi kama wakifanikiwa kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa barani Ulaya msimu ujao na sare waliyopata katika mchezo huo haijawaharibia sana kwani imewaacha katika nafasi ya nne mwa msimamo wa Ligi Kuu nchini Uingereza. 

No comments:

Post a Comment