Monday, April 29, 2013

RONALDO AKANUSHA KULALA NA 'MISS BUMBUM'.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo amekanusha vikali tuhuma za kumsaliti rafiki yake wa kike Irina Shayk kwa kutembea na mwanamitindo wa Brazil Andressa Urach ambaye anajulikana pia kwa jina ya ‘Miss BumBum’. Urach alikaririwa na gazeti la The Sun akidai kuwa alilala na nyota huyo wa Madrid katika hoteli ya Villa Magna saa 48 kabla ya mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Dortmund lakini nyota huyo amesisitiza kuwa hakuna ukweli katika hilo. Ronaldo aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa twitter akilalamikia kitendo cha mwanamitindo huyo kutaka kumchafua kwa kile kilichoandikwa katika gazeti hilo. Ronaldo aliendelea kuandika kuwa ni kweli alifikia katika hoteli hiyo Aprili 22 kwa ajili ya mahojiano lakini mengine yote yaliyozungumza baada ya hapo ni uongo na uzushi mtupu.

No comments:

Post a Comment