
Thursday, April 18, 2013
FUFA KUNTAJA KOCHA MPYA KABLA YA JUNI.
SHIRIKISHO la Soka nchini Uganda-FUFA limesema kuwa lina uhakika wa timu ya taifa ya nchi hiyo kupata kocha mpya kabla ya mechi zao mbili za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Liberia na Angola zitakazochezwa Juni mwaka huu. Nafasi ya kocha wa nchi hiyo maarufu kama The Cranes ilibakia wazi baada ya Bobby Williamson kutimuliwa wiki iliyopita. Ofisa Habari wa FUFA amesema ni matumaini yao kocha mpya atapatikana kabla ya mechi yao dhidi ya Liberia na anaamini hilo litatokea. Makocha mbalimbali wametuma maombi yao ya kutaka kibarua cha kuinoa The Cranes wakiwemo Dario Bonetti wa Italia, Nikola Kavazovic wa Serbia na Tom Sainfeit wa Ubelgiji ambaye pia amewahi kuinoa Yanga ya Dar es Salaam.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment