Thursday, April 25, 2013

GIROUD ASHANGAZWA NA UAMUZI WA FA.

MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Oliver Giroud amekishambulia Chama cha Soka nchini Uingereza-FA baada ya uamuzi wake wa kutupilia rufani yake ya kupinga kadi nyekundu aliyopewa. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alitolewa nje na mwamuzi Andre Marriner kwa kumchezea vibaya Stanislav Manolev wakati wa mchezo baina ya Arsenal na Fulham Jumamosi iliyopita hivyo kupelekea kufungiwa mechi tatu kwasababu ya kupewa kadi nyekundu ya moja kwa moja. Giroud mwenye umri wa miaka 26 amekuwa akijitetea kwamba aliteleza bahati mbaya kwenye tukio hilo na baada ya rufani yake kutupiliwa mbali amewakosoa FA kwa hatua waliyochukua. Giroud amesema ameshangazwa na hatua iliyochukuliwa na FA dhidi yake, sio kwamba imemuumiza ila anadhabu sheria za Uingereza zimekuwa kali sana ukilingasha na makosa yanayofanywa.

No comments:

Post a Comment