Thursday, April 25, 2013

MBONA AIWINDA NAFASI YA KUINOA INDOMITABLE LIONS.

MCHEZAJI wa zamani wa kimataifa wa Cameroon, Patrick Mboma ameonyesha nia yake ya kuifundisha timu ya taifa ya nchi hiyo na anakusudia kutuma maombi yake Shirikisho la Soka la Cameroon-Fecafoot siku moja baada ya Waziri wa Michezo Adoum Garoua kulitaka shirikisho hilo kufanya mchakato wa kupata kocha mpya. Mshambuliaji huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 42 alikuwemo katika kikosi cha nchi hiyo ambacho kilinyakuwa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2000 na 2002 na pia kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika. Hata hivyo Mboma hajawahi kufundisha timu yoyote na wadau wa soka nchini humo wamedai kuwa mshambuliaji huyo wa zamani wa Paris Saint Germain na Parma hana uzoefu wa kutosha wa kumuwezesha kupewa nafasi ya kuinoa timu hiyo. Lakini pamoja na wadau kuponda uwezo wake Mboma amesema haimkatishi tamaa na atatuma maombi yake kuiwinda nafasi hiyo.

No comments:

Post a Comment